Siku hiyo Webuye kulikuwa na huzuni nzito. Tulikuwa tumekusanyika kwa ajili ya mazishi ya ndugu yetu ambaye kifo chake kilikuja ghafla na bila maelezo ya kueleweka. Watu walinong’ona pembeni wakisema huenda kulikuwa na jambo lililofichika, lakini hakuna aliyekuwa na uthibitisho.
Mazishi yalianza kama kawaida maombi, hotuba, na maandalizi ya mwisho ya kumzika. Lakini mambo yalibadilika ghafla tulipofika wakati wa kushusha mwili kaburini. Kitu kisicho cha kawaida kilitokea. Kila walipojaribu kushusha jeneza, hali ilionekana kuwa ngumu kupita kawaida.




0 Comments