Subscribe Us

MHANDISI KWILASA NTARE, ACHUKUA FOMU KUOMBA RIDHAA YA UBUNGE NYAMAGANA

Mhandisi Kwilasa Deogratias Ntare  Mtia nia ridhaa ya ubunge Jimbo la Nyamagana.

..................................

Na Dotto Mwaibale 

MHANDISI Kwilasa Deogratias Ntare anaomba ridhaa ya kupitishwa na chama chake ili aweze kuteuliwa kugombea Ubunge Jimbo la Nyamagana kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) akishindana na Mbunge   aliyemaliza muda wake Stanslaus Mabula ambaye anatetea nafasi yake.

Ntare anakuwa ni mmoja wa makada wa chama hicho 26 watakaochuana na mbunge huyo aliye maliza muda wake anaye wania kipindi kingine cha tatu tangu alipo chaguliwa mwaka 2015 kushika nafasi hiyo. 

Mmoja wa watia nia wa nafasi hiyo atakaye chaguliwa na chama hicho na kushinda kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika oktoba mwaka huu atakwenda kuwahudumia wananchi wa kata 18 zilizopo katika jimbo hilo  ambazo ni Lwanhima,  Buhongwa , Mkolani, Luchelele, Nyegezi, Butimba, Mkuyuni na Igogo.

Kata nyingine ni Pamba, Nyamagana, Milongo, Mbugani, Mahina, Mhandu, Igoma, Mabatini, Kishili na Isamilo .

Ntare anatajwa kuwa ni mtia nia mwenye uzoefu wa masuala ya siasa kwani nafasi yake katika chama hicho ni Kamanda wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Kata ya Goba, Mjumbe wa Mkutano  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni akiwakilisha tawi la Kitongwa, Mjumbe wa Kamati ya Maadili tawi la Kitongwa na Mjumbe wa Kamati ya Siasa tawi la Kitongwa.

Kada huyo mbali ya kuwa mbobezi wa wa siasa pia ni mtaalamu wa masuala ya biashara ni Afisa masoko, Msimamizi wa mahusiano kwenye kampuni ya madini, W

wakala wa matangazo na ving'amuzi na mtaalamu wa kilimo.

Kwenye jimbo hilo Serikali imefanya kazi kubwa chini ya Rais Samia kupitia mbunge aliyemaliza muda wake Stanslaus Mabula, lakini kutokana na kuwepo kwa demokrasia ndio maana watia nia wengi wamejitokeza ili atayefanikiwa kuwa mbunge aweze kuendeleza  maendeleo kwenye maeneo  ambayo bado yana changamoto mbalimbali.

Jimbo la Nyamagana linahitaji kupata kiongozi bora mwenye uwezo, weledi, mbunifu, maono na msomi ambaye atawaunganisha wana Nyamagana kushiriki kila jambo na kulifanya liweze kupiga hatua kubwa ya maendeleo na kutekeleza kwa ufanisi ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2025/ 2030.Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Nyamagana, Deogratias Nakey (kushoto), akimkabidhi fomu Mhandisi Kwilasa Deogratias Ntare ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge Jimbo la Nyamagana lililopo Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Julai 1, 2025.

Post a Comment

0 Comments