Subscribe Us

CCM WILAYA YA BABATI MJINI WAVUNJA MAKUNDI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU 2025

Wana CCM wa Wilaya ya Babati Mjini wakionesha mshikamano baada ya kuvunja makundi kuelekea uchaguzi mkuu 2025.

.......................................

Na Mwandishi Wetu, Manyara 

Kamati ya  Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Babati mjini mkoani Manyara ikiongozwa na Mwenyekiti wake Elizabeth Malley wameendelea na ziara ya kuvunja makundi ya ubunge na udiwani ambapo walitembelea kata ya Bonga na Singe.

Mwenyekiti aliwataka waliokuwa wagombea kuwa kitu kimoja na kuwaunga mkono wote walioteuliwa kupeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi kwa nafasi ya ubunge na udiwani.

Aliwataka pia wana CCM kuendelea kushikamana kuelekea uchaguzi mkuu. 

Post a Comment

0 Comments