Subscribe Us

WAZEE HAWA WAPO KATIKA MAUMIVU MAKALI YA MARADHI WAOMBA MSAADA WA MATIBABU

Mzee Said Bakari Nyumbu (kulia) na Mzee Ally Abdallah Ngurungu wakazi wa  Mtaa wa Ngurungu , Maji Matitu (A) Mbagala Jijini Dar es Salaam wakiwa pamoja. Wazee hawa wanasumbuliwa na maradhi wanaomba msaada wa matibabu.

..................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

WAZEE Said Bakari Nyumbu (68) na Mzee Ally Abdallah Ngurungu (70) wakazi wa  Mtaa wa Ngurungu , Maji Matitu (A) Mbagala Jijini Dar es Salaam maisha yao yapo hatarini kufuatia maradhi yanayo wasibu na sasa wanategemea kudra tu za Mwenyezi Mungu wanaomba msaada wa matibabu..

Awali Mzee Ngurungu licha ya kuwa na changamoto za kiafya ndiye  aliyekuwa akimsaidia Mzee mwenzake Nyumbu ambaye hana ndugu anaishi kwa kusaidiwa na wasamaria wema baada ya bosi wake aliyekuwa akimsaidia kazi kushindwa kumsaidia kutokana na uzee.

Wazee hawa wanachangamoto ya maradhi ya utu uzima ambapo Mzee Nyumbu anachangamoto ya  usikivu hafifu, Tezidume na anakidonda katika moja ya kidole chake ambacho kila siku kimekuwa kikiongezeka na hivyo kumfanya akate tamaa ya kuishi.

Hivi sasa Mzee Nyumbu amelazwa Hospitali ya Rifaa ya Mkoa wa Temeke ambapo bado hajaanza kupatiwa matibabu zaidi ya kupewa dawa za kutuliza maumivu.

Kwa upande wa Mzee Ngurungu yeye anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari, miguu kupata ganzi, uoni hafifu na mwili kukosa nguvu.

Mzee Ngurungu anasema ameshindwa kwenda hospitali kwa kuwa hana fedha hivyo yupo tu nyumbani akiteseka kwa maumivu.

Ndugu watanzania hayo ndiyo madhira wanayopitia wazee wetu hawa ambao mimi naweza kuwaita mapacha kutokana na ukaribu walionao ambao umewafanya wafahamiane kutokana na changamoto walizonazo.

Wazee hawa licha ya kukabiliwa na changamoto hizo za maradhi pia wanachangamoto za mahitaji mengine ya kibinadamu kama chakula hivyo wanaomba msaada wa kupata matibabu na mahitaji hayo mengine.

Kama mtaguswa kuwasaidia hata Shilingi 2000 utakayokuwa nayo unaweza kuwasiliana na Mzee Ally Abdallah Ngurungu kwa namba ya simu 0784679755 au Mwandishi wa taarifa hii kupitia namba 0754362990 kwa maelezo zaidi.

Ndugu Watanzania kila mmoja kwa Imani yake wazee wetu hawa wamekwama wanahitaji msaada  kutoa ni moyo wa mtu na wala siyo utajiri.

Changamoto za Wazee hawa zimeibuliwa na Wajumbe wa Serikali ya Mtaa wa Matitu A ikiwa ni moja ya njia ya kutatua changamoto za wananchi wajumbe hao ni Hawa Omari na Jihadi Umwagala.

 

Wazee hao wakiwa pamoja Maji Matitu (A) Mbagala Jijini Dar es Salaam. 

 

Post a Comment

0 Comments