Subscribe Us

UVCCM BABATI MJINI WASAKA KURA KILA KONA

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Babati Mjini, Magdalena Urono akizungumza na wananchi (hawapo pichani) wakati walipokuwa wakiomba kura za wagombea wa chama hicho. Kulia ni Mgombea Ubunge Jimbo la Babati Mjini,  Emmanuel Khambay na kushoto ni Katibu wa Hamasa wa wilaya hiyo, Haji Ally,

............................................  

Na Mwandishi Wetu, Manyara

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Wilaya ya Babati Mjini unaendelea kwa kasi kusaka kura za wagombea wa chama hicho katika siku  chache zilizobaki kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025.

Akizungumza wakati wakiomba kura leo Oktoba 16, 2025 mwenyekiti wa umoja huo Wilaya ya Babati Mjini, Magdalena Urono alisema kasi ya kutafuta kura za wagombea wao imeongezeka ambapo wanapita kila kona walipowananchi kuwaomba kura zao kwa ajili ya CCM.

“Tupo na mgombea wetu wa nafasi ya ubunge jimbo la Babati mjini, Emmanuel Khambay tunapita kila kona walipo wananchi na makundi yaa vijana kuzisaka kura za wagombea wetu wote wa CCM kwa kweli wanatuelewa na wametuahidi kutupa kura, “ alisema Urono.

Alisema matamanio yao ni kuona wilaya hiyo inakuwa ya kwanza kwa kuwa na kura nyingi za mgombea nafasi ya urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, mbunge na madiwani.

Alisema wanazisaka kura huku wakielezea kazi kubwa iliyofanywa na Serikali kupitia ilani ya CCM ya 2020/ 2025 chini ya Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho Dkt. Samia kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mgombea ubunge wa jimbo hilo Emmanuel Khambay aliwaomba wananchi hao kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura za wagombea wa CCM na kueleza kuwa ndiyo chama pekee ambacho kimebeba maono ya maendeleo.

“Tuchagueni wagombea wote wa CCM kwani ndiyo chama chenye mipango mizuri ambayo inaenda kutekelezwa katika ilani ya uchaguzi ya 2025/ 2030,” alisema Khambay.

Mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Babati Mjini,  Emmanuel Khambay, akizungumza wakati akiomba kura.
Salamu zikitolewa kabla ya kuomba kura. Kutoka kulia ni Katibu Hamasa wa wilaya hiyo, Haji Ally, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Emmanuel Khambay, Mwenyekiti wa UVCCM wa wilaya hiyo, Magdalena Orono na kada wa chama hicho. 
Kura zikiombwa kwa wananchi (hawapo pichani)
 

Post a Comment

0 Comments