Subscribe Us

DC MKALAMA AIPONGEZA TAKUKURU SINGIDA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali, ambaye alikuwa mgeni rasmi akisisitiza jambo wakati akifungua Semina ya Maafisa Usafirishaji (Bodaboda) na Mawakala wa Huduma za Fedha wa Wilayani humo iliyofanyika Oktoba 22, 2025

.........................................

Na Dotto Mwaibale, Mkalama

MKUU wa Wilaya ya Mkalama mkoani Singida Mhe. Moses Machali, ameipongeza Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida kwa jinsi ilivyojidhatiti kukabiliana na vitendo vya rushwa.

Machali alitoa pongezi hizo Oktoba 22, 2025 wakati alipokuwa akifungua Semina ya Maafisa Usafirishaji (Bodaboda) na Mawakala wa Huduma za Fedha Wilaya ya Mkalama iliyofanyika Oktoba 22, 2025.

“ Nikiwa kama kiongozi wa Serikali kwa mujibu wa sheria napenda nitumie fursa hii kuupongeza uongozi mzima wa TAKUKURU kuanzia Mkoa na katika wilaya chini ya Mkuu wa Takukuru mkoa Sosthenes Kibwengo kwa kazi nzuri mnayoifanya ya kukabiliana na vitendo vya rushwa,” alisema Mhe. Machali.

Machali alisema hana tabia ya kumsifia mtu lakini pale anapofanya vizuri hasiti kufanya hivyo kwani wanafanya kazi kubwa na nzuri ya kuelimisha wananchi dhidi ya rushwa.

Aidha, Machali kwa niaba ya Serikali alitumia nafasi hiyo kuwapongeza maafisa usafirishaji (Bodaboda) na Mawakala wa Huduma za Fedha kwa kukubali mualiko wa TAKUKURU kwenda kuhudhuria semina hiyo ili waweze kuelimishana juu ya mapambano ya masuala rushwa.

Pamoja na mambo mengine Semina hiyo iliyoandaliwa na TAKUKURU Wilaya ya Mkalama  imelenga kuongeza uelewa kuhusu uwajibikaji, uwazi na mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa katika sekta ya usafirishaji (bodaboda) na kwa watoa huduma za kifedha hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Mhe. Moses Machali, akizungumza kwenye Semina hiyo.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, Petro Horombe. akizungumza
Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Mkalama, Yassin Mohamed akizungumza kwenye semina hiyo.

Mkuu wa Kituo cha Polisi Nduguti Mrakibu Msaidizi (ASP) Fedrick Magowa akizungumza na maafisa Usafirishaji na Mawakala wa Huduma za Fedha..

Maafisa Usafirishai wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa


Semina ikiendelea
Maafisa Usafirishaji (Bodaboda) wakiwa kwenye Semina hiyo.
 

Post a Comment

0 Comments