Subscribe Us

𝐖𝐀𝐋𝐈𝐌𝐔 𝐖𝐀𝐋𝐈𝐀 𝐑𝐀𝐅𝐔 𝐊𝐔𝐉𝐈𝐓𝐎𝐀 𝐂𝐖𝐓 𝐊𝐔𝐉𝐈𝐔𝐍𝐆𝐀 𝐂𝐇𝐀𝐊𝐀𝐌𝐖𝐀𝐓𝐀

Wakurugenzi, maafisa utumishi watajwa.
Muonekano wa Jengo la Utawala la Halmashauri ya Wilaya Singida
................................................

WALIMU Wanachama wa Chama cha Kutetea Haki na Maslahi ya Walimu Tanzania (CHAKAMWATA) wamelalamikia kitendo cha baadhi ya Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari wanaohamia kutoka Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kuzuiwa kujiunga na chama hicho ambacho kipo kwa mujibu wa sheria.


Wanaotuhumiwa kuwazuia walimu hao ni Wakurugenzi, Maafisa Utumishi Wakuu na Maafisa Utumishi Wasaidizi wa Halmashauri mbalimbali nchini.


Walimu hao wanadai kuwa licha ya kujiunga na CHAKAMWATA kwa kufuata hatua zote za kisheria, Maafisa hao wanaoingia kwenye mfumo wa mishahara yao (LAWSON) na wamekuwa wakikataa kuwaunga CHAKAMWATA walikojiunga badala yake wanawalazimisha wabaki CWT walikojitoa.


Maafisa hao wanadaiwa kukataa kuondoa makato ya 2% ya CWT na kuingiza michango ya 1% ya CHAKAMWATA kwenye mishahara ya Walimu wanaojitoa kutoka CWT na kujiunga na CHAKAMWATA.

KUENDELEA  KUSOMA

👉BOFYA   HAPA

Post a Comment

0 Comments