Subscribe Us

MBUNGE BABATI MJINI ASHEREHEKEA BOXING DAY NA WAHITAJI


Misa ya shukrani iliyofanyika Kanisa Katoliki Parokia ya Roho Mtakatifu Babati Mjini ambayo Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Emmanuel Khambay alihudhuria ikiendelea.

...............................

Na Mwandishi Wetu, Manyara

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini Mhe Emmanuel Khambay amehitimisha sherehe ya Krismasi kwa kushiriki chakula na wahitaji.

Mhe. Khambay ametumia siku ya pili baada ya sikukuu ya krismasi ‘Boxing Day’ ambayo ni maalumu kwa kufungua zawadi kusherehekea na wahitaji kwa kushirikiana na Vijana wa Katoliki wa Tanzania (VIWAWA) Parokia ya Roho Mtakatifu ambapo alitoa ng’ombe kwa ajili ya kitoweo.

Sherehekea hiyo iliyofanyika Desemba 26, 2025 iliwahusisha watoto yatima, watoto wanaoishi katika mazingira magumu ambayo ilikwenda sambamba  na Misa ya shukrani iliyofanyika Kanisa Katoliki Parokia ya Roho Mtakatifu .

Hafla hiyo ilifanyika Ufukwe wa Paradise uliopo Babati Mjini.

Akizungumza katika hafla hiyo Khambay alisema ataendelea kushirikiana na wahitaji katika masuala mbalimbali yanayowahusu na shughuli za maendeleo kutokana na kutambua mchango walionao katika jamii licha ya kuwa na changamoto mbalimbali.

Viongozi wa Viwawa na wahitaji wakizungumza kwa nyakati tofauti katika hafla hiyo walimshukuru Mhe. Khambay kwa kuandaa hafla hiyo na kuonesha jinsi anavyowajali ambapo walimuomba Mungu aendelee kumpa afya njema na maisha marefu ya kuwatumikia wananchi wa Babati na Taifa kwa ujumla.

Hafla hiyo ilinogeshwa na burudani za nyimbo za kumtukuza Mungu kutoka kwa Viwawa na wahitaji

Keki maalumu ya hafla ya Wahitaji, Viwawa na Mhe.Mbunge Kambay ikikatwa.
Viongozi wa Parokia hiyo na viongozi wengine wakilishwa keki hiyo.
Burudani za nyimbo za kumtukuza Mungu zikiimbwa.
Chakula kikigawiwa.
Kwaya ikitoa burudani.
Misa ya shukrani ikifanyika
Watoto wenye uhitaji wakipata chakula
Watoto wakipata chakula. 

Post a Comment

0 Comments