............................
Na Dotto Mwaibale
MBUNGE wa Jimbo la Babati Mjini, Mhe. Emmanuel Khambay kesho anatarajia kuanza ziara ya kikazi ya
kukagua shughuli za maendeleo pamoja na kuzungumza na wananchi.
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na ofisi yake kesho Januari
6, 2026 atafanya ziara hiyo Kata ya Singi eneo la Gendi Barazani na Januari 2,
2026 atakuwa Kata ya Nangara Kituo cha
afya.
Januari 8 atakuwa Kata ya Sigino na atakuwa na mkutano ofisi
ya Kata ya Sigino ambapo Januari 9 atakuwa Kata ya Mtuka ambapo pia atafanya mkutano ofisi ya kata
hiyo.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa Januari 10, Mbunge Khambay
atafanya ziara Kata ya Maisaka na kufanya mkutano ofisi ya kata hiyo ambapo
Januari 11 atakuwa Kata ya Bagara eneo la Nakwa na kuhitimisha ziara hiyo
Januari 12 Babati mjini eneo la Maisaka B na kutaja muda kuwa ni 8:00 Mchana.
Mhe. Khambay anawaalika wananchi wote kushiriki ziara hiyo.
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale 0754362990




0 Comments