Kwa zaidi ya miaka kumi, nimekuwa “malkia wa pete za uchumba.”
Nina mkusanyiko wa pete nne tofauti ndani ya sanduku langu, zote nilipewa na
wanaume walioahidi kunioa lakini kila harusi ilipokaribia, walikuwa wakitokomea
kusikojulikana au kuanza vitimbwi visivyovumilika.
Hali hii ilinifanya nionekane kama kichekesho mbele ya
wafanyakazi wenzangu. Kila mwaka shuleni nilikuwa nabadilisha “shemeji,” jambo
lililonifanya nianze kujihisi nina nuksi au laana ya vizazi. Nilianza kuogopa
hata kuvaa pete mpya nikipewa, maana nilihisi ni ishara ya kuachwa tena.
Nilihangaika sana kutafuta suluhu, nimezunguka kwa kila aina ya wataalam wa mitishamba nchini Tanzania nikijaribu kusafisha nyota yangu, lakini kila niliyemfuata alikuwa akichukua mshahara wangu na kuniachia patupu huku hali ikiwa ileile.




0 Comments