Katika kuadhimisha Siku ya Misitu Duniani sambamba na Siku ya Upandaji Miti Kitaifa iliyofanyika mkoani Lindi Region, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Emmanuel John Nchimbi, alitembelea banda la FWITC na kujionea kwa karibu shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na chuo hicho.
Ziara hiyo ilitoa fursa ya kipekee kwa viongozi kujionea ubunifu na umahiri unaooneshwa kupitia bidhaa zinazozalishwa chuoni hapo. Bidhaa hizo, zilizotengenezwa na wanafunzi na wakufunzi, zinaakisi kiwango cha juu cha utaalamu na ubunifu katika sekta ya misitu. Aidha, Makamu wa Rais alipatiwa maelezo ya kina kuhusu mafunzo yanayotolewa, yakilenga kuwawezesha vijana kwa vitendo, kukuza ajira, na kuchangia maendeleo ya sekta ya misitu pamoja na uchumi wa taifa kwa ujumla.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA...ardenkitomaritz




0 Comments