Nilianza kuhisi kuna kitu si cha kawaida kwenye uhusiano wangu. Mpenzi wangu alibadilika polepole alianza kuchelewa kurudi nyumbani, simu yake kuwa siri kupita kiasi, na mara nyingi alikuwa akijifungia chumbani kwa muda mrefu akidai anahitaji kupumzika. Nilijaribu kupuuza, nikijiambia labda ni msongo wa maisha tu.
Lakini usiku mmoja, kila kitu kilibadilika.
Nilikuwa nimeamka ghafla katikati ya usiku. Niliposikiliza kwa makini, nilisikia sauti ya kicheko cha chini kutoka chumbani. Kilichonishtua ni kwamba siku hiyo nilijua kabisa kuwa tulikuwa wawili tu ndani ya nyumba.




0 Comments