Subscribe Us

SERIKALI IMETOA TRILIONI 3.5 KUWAWEZESHA VIJANA-MAJALIWA


 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

............................................ 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali imefanikiwa kutoa kiasi cha shilingi trilioni 3.5 kufikia mwaka 2024 kwa ajili ya uwezeshaji wa vijana kiuchumi kutoka shilingi bilioni 904 mwaka 2021. 

Amesema kuwa fedha hizo zimewasaidia vijana kupata mitaji ambayo imewawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za uzalishaji mali na hatimaye kuinua vipato vyao pamoja na uchumi wa Taifa. 

Amesema hayo leo Ijumaa (Oktoba 10, 2025) wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Vijana Kitaifa iliyofanyika mkoani Mbeya. Kaulimbiu ya Maadhimisho hayo ni Nguvu Kazi ya Vijana kwa Maendeleo Endelevu.”

Post a Comment

0 Comments